Korea Kaskazini yaionya Marekani kufuatia vikwazo vya UN Korea Kaskazini imeapa kulipiza kisasi na kuhakikisha kuwa Marekani imelipia gharama, kwa kubuni vikwazo vya Umoja wa Mataiafa kufuatia na mpango wake wa silaha za nuklia. Vikwazo hivyo vilivyoungwa mkono kwa kura nyingi na Umoja wa Mataifa siku ya Jumamosi "ni ukiukaji ya uhuru wa nchi," shirika la serikali la habari la Korea Kaskazini KCNA lilisema. Kwa upande mwingine Korea Kusini inasema kuwa Korea Kaskazini imekataa ombi la kutaka wafanye mazungumzo. Vikwazo hivyo vililenga kuzuia mauzo ya bidhaa za Korea Kaskazini kwa theluthi moja. Uamuzi huo wa Halmashauri ya Usalama wa Umoja wa Mataifa ulitokana na majaribio ya kutupa makombora ya mara kwa mara na Korea ya Kaskazini, jambo ambalo limechangia kuongezeka kwa wasi wasi kwenye rasi Korea. Katika jibu lake kuu la kwanza Jumatatu, Korea ya Kaskazini imesisitiza kuwa itaendelea kuendeleza mpango wake tata wa silaha za nyuklia. Shirikisho la habari la KCNA lina...
Mbegu za maboga zina protini na madini ya kutosha na ya mhimu zaidi mwilini kama madini ya zinki, kopa, maginizia, manganizi na chuma, mbegu za maboga ni tamu na zinaweza kutafunwa nyakati zozote na mahali popote hasa kwa wapenda kutafuna-tafuna kama mimi. Tafiti mbalimbali zimethibitisha pasipo na shaka kuwa mbegu za maboga zina faida nyingi kiafya na zina uwezo wa kukuepusha na magonjwa hatari zaidi ya 10 yafuatayo: 1. UGONJWA WA MOYO Kiasi kingi cha madini ya magnesium katika mbegu za maboga yanazifanya mbegu hizi kuwa mhimu sana kwa watu wenye magonjwa mbalimabli ya moyo. Madini ya magnesium ni mhimu kwa ajili ya kuimarisha msukumo wa damu kwenye moyo na kuimarisha afya ya mishipa ya damu hatimaye kutibu na kuzuia magonjwa ya moyo. Mbegu hizi pia zina mafuta mengine mhimu zaidi kwa watu wenye ugonjwa wa moyo yenye OMEGA 3. 2. HUIMARISHA KINGA YA MWILI Mbegu za maboga zimebarikiwa kuwa na kiasi cha kutosha cha madini ya zinki (zinc). Kazi kubwa ya madini ya zink ...