Skip to main content

Posts

Korea Kaskazini yaapa kulipiza Kisasi kwa Marekani.

Korea Kaskazini yaionya Marekani kufuatia vikwazo vya UN Korea Kaskazini imeapa kulipiza kisasi na kuhakikisha kuwa Marekani imelipia gharama, kwa kubuni vikwazo vya Umoja wa Mataiafa kufuatia na mpango wake wa silaha za nuklia. Vikwazo hivyo vilivyoungwa mkono kwa kura nyingi na Umoja wa Mataifa siku ya Jumamosi "ni ukiukaji ya uhuru wa nchi," shirika la serikali la habari la Korea Kaskazini KCNA lilisema. Kwa upande mwingine Korea Kusini inasema kuwa Korea Kaskazini imekataa ombi la kutaka wafanye mazungumzo. Vikwazo hivyo vililenga kuzuia mauzo ya bidhaa za Korea Kaskazini kwa theluthi moja. Uamuzi huo wa Halmashauri ya Usalama wa Umoja wa Mataifa ulitokana na majaribio ya kutupa makombora ya mara kwa mara na Korea ya Kaskazini, jambo ambalo limechangia kuongezeka kwa wasi wasi kwenye rasi Korea. Katika jibu lake kuu la kwanza Jumatatu, Korea ya Kaskazini imesisitiza kuwa itaendelea kuendeleza mpango wake tata wa silaha za nyuklia. Shirikisho la habari la KCNA lina...
Recent posts

Fahamu namna ya kujitibu/kujikinga kwa mbegu za maboga

Mbegu za maboga zina protini na madini ya kutosha na ya mhimu zaidi mwilini kama madini ya zinki, kopa, maginizia, manganizi na chuma, mbegu za maboga ni tamu na zinaweza kutafunwa nyakati zozote na mahali popote hasa kwa wapenda kutafuna-tafuna kama mimi. Tafiti mbalimbali zimethibitisha pasipo na shaka kuwa mbegu za maboga zina faida nyingi kiafya na zina uwezo wa kukuepusha na magonjwa hatari zaidi ya 10 yafuatayo: 1. UGONJWA WA MOYO Kiasi kingi cha madini ya magnesium katika mbegu za maboga yanazifanya mbegu hizi kuwa mhimu sana kwa watu wenye magonjwa mbalimabli ya moyo. Madini ya magnesium ni mhimu kwa ajili ya kuimarisha msukumo wa damu kwenye moyo na kuimarisha afya ya mishipa ya damu hatimaye kutibu na kuzuia magonjwa ya moyo. Mbegu hizi pia zina mafuta mengine mhimu zaidi kwa watu wenye ugonjwa wa moyo yenye OMEGA 3. 2. HUIMARISHA KINGA YA MWILI Mbegu za maboga zimebarikiwa kuwa na kiasi cha kutosha cha madini ya zinki (zinc). Kazi kubwa ya madini ya zink ...

Magufuli; Anna Mghwira ana uwezo wa kuchapa kazi.

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amemuapisha aliyekuwa mgombea urais mwaka 2015 Bi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na kusema anaweza kuitekeleza kazi hiyo. Bi Anna Elisha Mghwira amejaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadiki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo ambaye aliacha kazi. Akizungumza baada ya kumuapisha, Rais Magufuli amemtaka Bibi Anna Elisha Mghwira kwenda kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuondoa kero zinazowakabili wananchi wa Kilimanjaro bila kujali itikadi za vyama vyao vya siasa, dini, makabila na kanda wanazotoka. Alisema anaamini mwanasiasa huyo ana uwezo wa kutekeleza majukumu yanayoambatana na kazi hiyo. "Mimi huwa siteui watu hivi hivi, huwa naangalia uwezo wa mtu, na wewe nimekuchunguza na nimejiridhisha kuwa una uwezo wa kuwatumikia wananchi, nenda kachape kazi, kawaondolee kero wananchi wa Kilimanjaro, wapo watu watakaokusema na wengine watakuonea wivu, wewe kachape kazi," amesema Dkt Magufuli, baada ya kumuapis...

Wanafunzia shule ya msingi Maretadu waangukiwa na kifusi.

Kuna habari ya kusikitisha nimeipata kwamba, ajali mbaya imewachukua wanafunzi Maretadu mkoani Manyara. Wanafunzi hao wa shule ya msingi Maretadu Chini, waliangukiwa na kifusi hapo pichani katika Korongo, kitongoji cha Gidif.  Wawili walifariki palepale na mmoja kalazwa Hospitali ya Haydom na hali yake inaendelea vizuri.              Chanzo: Jamii forum .

Lowasa afunguka kuhusu madai ya kutovaa sare za CHADEMA.

Si kweli kuwa sivai sare za CHADEMA, hata nilipokuwa CCM nilikuwa nashona shati la rangi moja ama kijani au njano kisha naweka nembo maalumu ya chama, vivyo hivyo hata CHADEMA naweka nembo maalum. " Na jambo kubwa hapa ni kuwa, nisihukumiwe kwa kuvaa au kutokuvaa sare za CHADEMA lakini kwa matendo yangu." Hayo ni maneno yaliyotolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Ngoyai Lowassa alipokuwa akijibu swali la mtangazaji wa kituo cha Azam Tv, Charles Hillary aliyetaka kujua kwanini havai sare za CHADEMA katika matukio mbalimbali kama ilivyokuwa CCM. Lowassa alienda mbali na kusema kuwa, sare si jambo kubwa sana kwani mtu anaweza kuvaa sare na bado akawa si mmoja wenu. Unaweza kukuta mtu kavaa nguo za kijani lakini kiukweli moyoni si wa CCM Aidha, Lowassa alisema, alipomaliza Chuo Kikuu alikwenda jeshini na kwa muda wote huo alikuwa akivaa magwanda, hivyo alishavaa vya kutosha, na umri wake kwa sasa si wa kuvaa tena....